Ads (728x90)

Tabs

Page

IMG_0118-630x360
Nahodha wa Mbeya City Fc  Hassan Mwasapili amesema  2015/16 ndiyo msimu ambao timu yake itaandika historia mpya  ya kushiriki michuano ya kimataifa inayoandaliwa na shirikisho la soka barani afrika CAF.
 Mwasapili ameiambia Tovuti ya Mbeya City kuwa City imekuwa na mafanikio mazuri  kwenye soka la Tanzania tangu ilipopanda daraja kwa mara ya kwanza 2013/14 na imefanikiwa kuwa sehemu ya timu nne za juu kwa miaka miwili mfululizo kwenye msimamo wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara hivyo ina  nafasi kubwa ya kusogea zaidi hasa ya  uzoefu wa miaka hiyo.
“Misimu miwili imetupa uzoefu wa kutosha, licha ya ugeni tumekuwa kwenye nafasi nne za juu muda wote tulioingia kwenye ligi, huu ni wakati wa kucheza michuano ya CAF, nia yetu ni kuweka rekodi nyingine  msimu huu mpya, timu yetu bado iko vizuri licha ya wachache kuondoka, mwalimu amepandisha vijana saba wenye vipaji vikubwa imani yangu wanakuja kufanya makubwa pengine kuliko walioondoka ambao nao walikuwa vijana wadogo kama hawa wakati wanaingia City”  alisema Mwasapili

Post a Comment