Ads (728x90)

Tabs

Page

Podolsk
Wakati hekaheka za usajili zikiwa zimepamba moto barani Ulaya, wababe wa soka nchini Uturuki Galatasaray, wamethibitisha  kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Bayern Munich na Inter Milan Lukas Podolski kwa ada ya pauni
milioni mbili na nusu.
Podolski ,30, ambaye alijiunga na Arsenal miaka mitatu iliyopita amekuwa na wakati mgumu klabuni hapo mara baada ya kukosa nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza, hali iliyopelekea kutolewa kwa mkopo kwenda Inter Milan ya nchini Italia.
“Tulikuwa na mazungumzo mazuri na Wenger,” Touihri aliliambia gazeti la Bild la nchini Ujerumani.
“Bado alitaka kumbakisha Lukas klabuni lakini alishindwa kumhakikishia nafasi katika kikosi cha kwanza. Ndio maana tukafikia muafaka katika  zoezi hili.”
Podolski amefunga mara mbili dhidi ya Galatasaray katika mchuano ya vilabu bingwa Ulaya msimu uliopita

Post a Comment