Ads (728x90)

Tabs

Page


Kundi maarufu la muziki kutoka Nigeria P Square wanazidi kuvuna mafanikio yao mengi wanayoyapata kupitia muziki… hivi karibuni kundi hilo lilipata fursa ya kutembelea ofisi za rapper Jay Z nchini Marekani, New York na kufanya nae interview pamoja na mkutano!
PSQUARE3
Peter Okoye wa P Square.
P Square walikuwa nchini Marekani kwa ajili ya tour na baada ya kurudi nyumbani Peter Okoye mmoja ya wasanii wanaounda kundi la P Square alichukuwa time na kupost kwenye account yake ya Instagram miongoni mwa mafanikio walioyapata kwenye tour ya safari hii huko Marekani kwa kupost picha na ujumbe uliosema…
>>> “Kwenye ofisi za @tidal na ilikuwa interview na mkutano poa sana. #SomethingBig #RocNations”.<<< @peterpsquare.
PSQUARE
P Square wakiwa kwenye ofisi za Jay Z Roc Nation/Tidal nchini Marekani hivi karibuni.
Miezi michache iliyopita Jay Z alimtuma binamu yake Bee High huko Nigeria kwenda kutafuta soko na wasanii ambao watakuwa tayari kufanya biashara na rapper huyo kupitia service na application yake ya kusikiliza na kudownload muziki TIDAL… Akiwa Nigeria Bee High alifanikiwa kukutana na Don Jazzy boss wa lebo ya Mavin Records, MI Abaga boss wa lebo ya Chocolate City pamoja na P Square wenyewe.

Post a Comment