Ads (728x90)

Tabs

Page

Tukiwa bado kwenye headlines za Uchaguzi 2015 stori ninayotaka kukusogezea ni hii kutoka kwa Diamond Platnumz ambaye amekuwa ni miongoni kati ya wasanii sera za wagombea katika majukwaa mbalimbali.
Msanii huyo alipokuta na Millardayo aliweza kueleza sababu zilizomfanya kuendelea kusupport kampeni za wagombea katika kipindi hiki cha Uchaguzi na kusema…‘Kiukweli siwezi kusema ni changamoto kwangu ila naona tu kuna baadhi ya watu ambao hawataki kukubaliana na ukweli na usawa wangu mimi na uamuzi wangu mimi kwasababu mimi ni mtanzania ni mtu pia ambaye nataka maendeleo kama watu wengi na ukiangalia tangu naanza wimbo wangu wa kwanza nenda kamwambie natoa Mbagala nikaubadilisha nikaimba CCM’ – Diamond Platnumz
Maana naona kuna baadhi ya watu wanasema mara Diamond utapotea sasa mimi na Marlaw tuko mstari wa mbele nimeshafanya kampeni ya kwanza Kikwete akiingia madarakani na kile sababu ya kujiamini na kuichagua CCM labda ingelikuwa kipindi kile Mheshimiwa Zitto Kabwe yuko kule Zitto ametusaidia sana katika sanaa pia hata mimi amenisaidia ana mchango mkubwa sana’ -Diamond Platnumz
‘Kwa hiyo huyo ni moja kati ya wanasiasa ambaye anajalia na kudhamini mtu, ku support chama haiwezi kuchafua brand yangu  kwasababu mwisho wa siku hivi vitu tunavyovifanya watu tu wataenda kupiga kura na Rais atapatikana wa Ikulu na sidhani kama mtu atapata nafasi ya kuingia Ikulu labda wasanii tu kwa hiyo hivi ni vitu tu tunaleta ushabiki kama timu za mpira’ – Diamond Platnumz
Kwa hiyo mtu akisema ananikasirikia mimi kisa nashabiki CCM ningependa kusema hizi ni siasa tu, kwa upande wa wasanii kuna Ney, Wolper, Shamsa hao ni marafiki zangu tena hakuna mtu asiyejua urafiki wangu na Ney hizi ni siasa tu kubishana mwisho wa siku maisha yanaendelea’ – Diamond Platnumz

Post a Comment