Ads (728x90)

Tabs

Page

Leo November 20 moja ya post ambazo zilikuwa reposted mara nyingi sana kwenye Instagram ni list ya Top 10 MCs of all time ambayo imetengenezwa na rapper Nikk Wa Pili. Baada ya ku-post baadhi ya watu walikua wanabisha kwenye comments na wengine wanakubaliana naye.
Hizi hapa ni sababu kwa kila mtu ambae amemtaja kwenye list yake. Nikk Wa Pili amezitoa sababu hizo kama hivi…
1) Sugu
Kwasababu yeye ndie foundation ya HipHop, alianza kutoa album na alianza kufanya live show. Niliwai kumshudia Sugu anafanya live show nyimbo 20. Harafu kila kitu ambacho MCs wanasema sasa hivi Sugu aliwai kusema kwa njia nyingine.
2)Profesa Jay
Jay alifanya break through ya Hiphop baada ya Sugu kuweka foundation. Jay alipeleka Hiphop kila mkoa hadi kwenye kila nyumba ikafika. So baada ya Sugu lazima afuatie Jay
3)Mangwea
Ngwea aliongeza fan base ya Hiphop hadi watu ambao ulikua hautegemea wangesikiliza Hiphop walianza kusikiliza Hiphop. Mangwea alifanya Hiphop ipigwe kwenye clubs na joints mbalimbali. Pia hadi wakina dada walianza kununua album ya Hiphop kwa Mangwea kwasababu aliifanya imekua sweet. Ukiacha uandishi wake lakini kuongeza fan base na kuifanya kuwa sweet.
4)Joh Makini
Most stylish MC, ukizungumzia style ya ku-ryhme yeye ndio symbol. Kuanzia anatoka na Hao hadi leo ametoa Don’t Bother hapo katikati kuna style nyingi sana za ku-flow amezifanya kwenye ngoma zake.
5)Mwana FA
FA alikuja kuongea upande mwingine wa stoei, alianza kuongea mapenzi kwenye Hiphop na zikawa big hit tofauti na ilivyokua. Tulizoea wakina Jay kuimba mambo ya serikalini lakini hatukuwa na mapenzi yaliyo kick kwenye Hiphop hadi ngoma za Mabinti Dam Dam zinatoka chini ya Mwana FA.
6)Fid Q
Huyu jamaa alikuja na style ya kusikia mstari mmoja lazima ufikirie. Pia mstari mmoja unaweza kuwa na maana zaidi ya tatu. Hii ilikua ni style ya pekee kabisa ya kufikisha ujumbe, mtu kama Jay alikua anachana direct massage kutoka mwanzo hadi mwisho lakini Fid alikua lazima afunge ili uweze kufikiria. Kwa hiyo ali-introduce kitu kipya kwenye Hiphop.
7)AY
Ambwene alileta biashara kwenye Hiphop na kuifanya kuwa bidhaa, alianza kuuvusha muziki kwenye nchi nyingine kabla ya mtu mwingine. Kama unakumbuka ukizungumzia muziki wa Tanzania ndani ya Nairobi ulikua unabebwa na A.Y. Hizi video za kali na collabo zote alizianzisha yeye.
8)Lord Eyes
Ukitaka kujua hard story za geto lazima umsikilize Lord Eyez. Huyu jamaa alikua anatoa story za geto hakuna zaidi yake yeye, wengine walikua wanachana ila kwa kuficha ficha lakini yeye alikua anaeleza uhalisia wa geto lilivyo, style yake ya kuchana ya kihuni kutoka mtaani ni identity tosha kabisa na hakuna takaye weza kuwa kama yeye.
9)Jay Mo
Ukizungumzia swala la story telling kwenye Hiphop Jay Mo ndio baba, ngoma kama maisha ya boarding, story tatu yeye ndio alifanikiwa sana kwenye uandishi na flow za Hiphop kwa upand wa story telling
10)Nikk Wa Pili
Ameingia hapa kwa sababu moja tu, ukizungumzia new generation ya Hiphop yeye ndiye number one.

Post a Comment