Ads (728x90)

Tabs

Page

dc
Moja ya mechi iliyoteka macho ya watu siku ya Jumamosi Nov 21 ni kati ya Juventus Vs AC Milan ambapo Juve ilishinda kwa magoli 1-0.
Kipa wa Juve Gigi Buffon hakupewa changamoto yoyote ya mipira mikali ya ku-save hadi kipindi cha pili kilivyofika.
“Kwenye mechi tulifanya makosa mengi sana, tulipata counter attacks lakini zilikua hovyo pia”, kocha Mihajlovic alisema.
Lakini Mihajlovic alikubali kwamba kuifunga Juventus bado ni ngumu hasa wakiwa Turin. Zaidi Mihajlovic alimzungumzia striker Niang, “Alifanya vizuri kwenye defensive lakini yeye ni striker na lazima afanya zaidi kwenye attacking. Ilikua ni mechi yake ya 2 ndani ya miezi minne au mitano, kwa hiyo anatakiwa level yake ya kuwa fit inatakiwa kuendelea ku-improve”
“Nawataka wachezaji wangu wajitoe sana wenyewe kwa ajili ya timu na wawe fit kwa ajili ya timu”.
Walioangalia hii mechi kupitia Startimes wanaelewa vizuri nini kocha huyu anamaanisha baada ya matokeo ya Juve 1-0 Ac Milan. Ligi ya Italy inaonekana Live kwenye king’amuzi cha Startimes, usipitwe na kila hatua ya ligi hii.

Post a Comment