Ads (728x90)

Tabs

Page

PORTO ALEGRE, BRAZIL - JUNE 15:  Karim Benzema of France celebrates after scoring his team's third goal during the 2014 FIFA World Cup Brazil Group E match between France and Honduras at Estadio Beira-Rio on June 15, 2014 in Porto Alegre, Brazil.  (Photo by Paul Gilham/Getty Images)
PORTO ALEGRE, BRAZIL - JUNE 15:  Karim Benzema of France celebrates after scoring his team's third goal during the 2014 FIFA World Cup Brazil Group E match between France and Honduras at Estadio Beira-Rio on June 15, 2014 in Porto Alegre, Brazil.  (Photo by Paul Gilham/Getty Images)
Nyota wa Real Madrid Karim Benzema amepigwa stop kuchaguliwa kwenye timu ya taifa ya Ufaransa hadi pale uchunguzi wa sakata lake linalohusisha kutaka kuvujisha video ya ngono inayomhusu Mathieu Valbuena utakapokamilika, Rais wa shirikisho la soka la Ufaransa Noel Le Graet amethibisha.
“Kuanzia leo, Benzema hatakiwi kuchaguliwa kwenye kikosi cha timu ya taifa”, Le Graet aliwaambia waandishi wa habari.
“Ninafahamu mtasema, lakini ni kipindi cha Christmas hivyo hakuna mechi, lakini zitakuwepo mwezi March”.
“Kama hakutakuwa na mabadiliko yoyotwe mwezi March (ambapo kutakuwa na mechi za kimataifa) hatocheza. Mtasema lakini kuna michuano ya Euro na mnampenda mchezaji huyu, hiyo itawavunja mioyo”.
Ufaransa itacheza na Uholanzi mchezo wa kirafiki wa kimataifa 25 March, 2016.

Post a Comment