Ads (728x90)

Tabs

Page


Tukiwa tumemaliza headlines za Uchaguzi Mkuu 2015, mwigizaji Frank alijitokeza kugombea Ubunge jimbo la Tabata Segerea kupitia tiketi ya ACT-Wazalendo lakini kutokana na kura zake kuwa chache hakufanikiwa kuwa mshindi wa jimbo hilo.
Akiongea na ripota wa millardayo.com mwigizaji huyo alisema…’Nilikuwa mgombe ubunge jimbo la Segerea kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, ingawaje sikuwa mshindi lakini naimani wamempokea vizuri mshindi  Bonnah Kaluwa…! Na nimekubali matokeo’– Frank
frank
Bado naonekana nina deni kwa wale walionipigia kura kama wawakilishi wa wana Segerea, hivyo kuna baadhi ya mambo yaliyo ndani ya uwezo wangu nitayafanya kwa wananchi wangu‘- Frank
Kulikuwa na changamoto nyingi, ingawa najipanga upya mwaka 2020 kugombea tena…! Ili kuweza kusaidi matatizo kama tatizo la maji, ujasiriamali, ajira, michezo na afya‘-Frank

Post a Comment