Ads (728x90)

Tabs

Page

Tumezoea kuona majeneza yakitumika kuhifadhia miili ya Marehemu au watu waliofariki, uliwahi kufikiria kuna mtu anaweza kutumia jeneza kwa biashara zake nyingine ?!!
Stori kwenye vichwa vya habari Kenya, jamaa watano wamenaswa wakiwa kwenye mchakato wa kusafirisha pombe haramu iliyopakiwa ndani ya jeneza, safari yote njiani wameenda wakiwa wanaomboleza kama watu wanaosafirisha msiba !!
Kenya II
Kenya kumekuwa na stori nyingi sana mfululizo zinazohusu watu kufariki, wengine kuumwa na wengine waliwahi kuripotiwa kupata tatizo la upofu kwa sababu ya unywaji wa pombe za kienyeji.. hiyo ilifanya Serikali ipige MARUFUKU utengenezwaji wa pombe hiyo.
Stori kamili hii hapa kutoka Kituo cha KTN Television cha Kenya mtu wangu, ni video ya dakika 2:39 tu.

Post a Comment