Ads (728x90)

Tabs

Page

Uwanja wa Stamford Bridge ni moja ya viwanja maarufu duniani katika mchezo wa soka, huu uwanja unamilikiwa na vigogo wa soka Chelsea.
Uongozi wa klabu hiyo tayari umewasilisha maombi ya mpango wake wa kupanua uwanja wao ili uweze kuingiza mashabiki 60,000 kwa wakati mmoja.
NDANI
Pamoja na maombi hayo tayari manispaa ya London Borough of Hammersmith na Fulham imekaribisha maoni toka kwa wananchi ili watoe ridhaa yao au pingamizi kabla ya kuruhusu upanuzi wa uwanja huo ambao utalazimu kubomoa baadhi ya majengo yaliyo karibu na uwanja huo.
CHESE
Chelsea, walianza kutumia uwanja wa Stamford Bridge, tangu 1905 ambapo mara ya mwisho kukarabatiwa na kupanuliwa ilikua mwaka 1990 na kuufanya uwe na uwezo wa kuchukua watazamaji 42,000.
Endapo ujenzi huo utaanza utamalizika mwaka 202o na utatumia kiasi ya Euro milioni 600.

Post a Comment