Ads (728x90)

Tabs

Page

Madee akizungumza kabla ya kuanza kwa mchezo Mabgufuli Cup #Hapa Kazi Tu kati ya Goms United dhidi ya Kauzu FC

Madee akizungumza kabla ya kuanza kwa mchezo Mabgufuli Cup #Hapa Kazi Tu 
Msanii kutoka kundi la Tip Top Connections Madee maarufu pia kwa jina la ‘Rais wa Manzese’ ambao ndio wandaaji wa michuano ya Magufuli Cup #Hapa Kazi Tu amesema amefurahi kutokana na mashindano hayo kuwa na mwamko mkubwa kwa kuwaleta watu tofauti pamoja kwenye viwanja zinapopigwa mechi za michuano hiyo.
“Nimefurahi mwamko umekuwa mkubwa kadri siku zinavyozidi kwenda mbele, viwanja vinajaa sana watu hamasa imekuwa kubwa halafu tunazidi kuona vipaji ambavyo watu hawajaviona bado na havijamulikwa na vyombo vikubwa”, amesema Madee.
“Kupitia Magufuli Cup tumewaona watu wengi na tunaamini baada ya hapa tutawasikia na kuwanaona kwenye ligi kubwa”.
“Mashindano yamekuwa magumu maana hata hizo timu zilizofuzu hazijafuzu kirahisi, kwa mfano Abajalo na Burudani zote zimefuzu kwa tofauti ya goli moja tu. Na toka tumeanza mashindano haya hakuna timu ambayo imeshinda zaidi ya magoli matatu”.
Katika hatua nyingine Madee anaipa nafasi timu ya Abaja kufanya vizuri kwenye michuano hiyo  kutokana na kuonesha kiwango kizuri kwenye mechi zake mbili za kwanza dhidi ya Zakhem ambapo ilifanikiwa kushinda mchezo wa kwanza kwa goli 2-1 ikiwa kwenye uwanja wa Mwl. Nyerere kabla ya kutoka sare ya kufungana kwa goli 1-1 kwenye uwanja wa Zakhem Mbagala.

Post a Comment