Ads (728x90)

Tabs

Page



Shirika la utafiti la saratani la WHO (IARC), limefanya uchambuzi wa kitafiti wa jinsi matumizi ya nyama nyekundu iliyosindikwa kuwa kisababishi cha saratani. Nyama iliyosindikwa ni ile iliyoongezewa kemikali za kuifadhi isiharibike na yaweza  kudumu kwa muda mrefu.

Lakini hii haimaanishi kuacha kula nyama kabisa, bali ni kuepuka nyama zilizosindikwa mfano nyama za makopo. Ripoti hiyo inasema kuwa, ulaji wa kadirio la gramu 50 za nyama iliyosindikwa itakuweka katika hatari ya kupata
saratani ya utumbo mkubwa.
Nyama ni mojawapo ya kirutubisho muhimu chenye protini inayohitajika kujenga mwili kwa hiyo hii haimaanishi kuacha kula nyama, bali kupunguza matumizi ya ulaji wa nyama nyekundu pamoja na nyama zilizosindikwa.
Ripoti hii inatokana na ushahidi wa kitafiti na wa kisayansi uliofanyika, na kulifanya shirika la afya duniani (WHO) kutoa tahadhari ili kuwaepusha watu na maradhi haya hatari yanayotishia afya za watu wengi ulimwenguni.

Post a Comment